top of page
Mafundisho


NYAKATI YA SABA YA KANISA, LAODIKIA
Kurudi kwa karama ikawa jambo geni katikakati ya waamini wengi kwa sababu zilikuwa zimekufa katika kanisa, zilibaki hadithi tu, na kurudi kwake ikawa ishara kama ila ya Pentecoste. Na tangu wakati ule yaani mwaka 1906 BK, wapentekoste tunaowajua leo wakazaliwa. Uamsho huu ulichukua mda mfupi kufika ulimwengu wote kuliko nyakati zote. Hivyo kila dhehebu la kipentekoste chimbuko lake ni huyu Wiliam Seymour. Ibada na mafundisho yakatijikita katika karama.
Dec 13, 20259 min read


NYAKATI YA SITA YA KANISA, FILADELFIA
Hao waliokuwa wa sinagogi la shetani ni kanisa la Katoliki. Kama nilivyotangulia kusema Anglican ni wakatoliki waliojitenga kwa sababu ya Mfalme Henry VIII mwaka 1534 BK. Na John wesley akaja kuwa kasisi mwaka 1728 BK. Na Anglican walikuwa na desturi nyingi za katoliki, ndio maana hawakuweza kuendana na mafundisho ya Wesley hata ikapelekea waumini wa John Wesley kuitwa wamethodist na si wa-anglican.
Dec 13, 20255 min read


NYAKATI YA TANO YA KANISA, SARDI
Malaika wa kanisa la tatu Martin wa tours na malaika wa kanisa la nne Columban wana tajwa na dhehebu la Katoliki hata leo kuwa ni watakatifu kwa sababu hawakupinga unikolai na ubalaamu ndani ya kanisa. Lakini Martin Luther hayupo katika orodha ya dhehebu lao ijapokuwa alikuwa na daraja la upadre, ni kwa sababu hakuridhia mafundisho yao ya wanikolai.
Dec 12, 20256 min read


NYAKATI YA NNE YA KANISA, THIATIRA
Yezebeli alikufa miaka mingi kabla ya maneno haya ya kitabu cha ufunuo kuandikwa, hivyo mwanamke huyu hana uhusiano wowote na kilichoandikwa, lakini Yezebeli anayezungumziwa hapa ni kanisa. Kwa sababu Mwanamke hufunua kanisa, dhehebu au dini fulani. Hivyo Columban alilidhia mafundisho ya kanisa ambalo linaenda kwa mafundisho kama yale ya Yezebeli, kuwafanya watu walioacha dhambi wairudie dhambi kana kwamba ni kumheshimu Mungu.
Nov 15, 20256 min read


NYAKATI YA TATU YA KANISA, PERGAMO.
Fundisho lingine lilikuwa kuheshimu wanadamu (watakatifu waliokufa) zaidi kuliko injili zao au matendo yao. Hii ilipelekea kuwatumikia wafu kwa kazi zao walipokuwa hai badala ya kumtumikia Mungu kama wao au kwa mfano wa matendo yao. Inaitwa kusujudia watakatifu waliokufa (Veneration). Maana ni sawa na mtu aliyeokota ganda la ndizi akalipanda katika nchi akitazamia litazaa ndizi.
Nov 6, 20256 min read


NYAKATI YA PILI YA KANISA, SIMIRNA.
Tunatazama kanisa la pili baada ya Efeso, yaani nyakati ya pili ya kanisa. Au kutakaswa kwa kanisa la kwanza. Kumbuka kanisa la kwanza liliacha upendo wa kwanza. Hivyo Bwana Yesu ili kuwatakasa kosa la kupungua kwa upendo aliwajaribu ikiwa bado wanampenda, Haya ndiyo aliyoyasema Yesu Kristo kwa kanisa hili la Smirna, Ufunuo wa Yohana 2:8-11. Ufunuo wa Yohana 2 ⁸ Na kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika; Haya ndiyo aneneyo yeye aliye wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa am
Oct 17, 20253 min read


NYAKATI YA KWANZA YA KANISA, EFESO.
Ndipo kwa sababu hiyo aliuacha upendo wa kwanza, alikuwa sahihi kabisa kumkemea Petro, na kila alichokuwa anakifanya lakini naye akaanza kupoa mwishoni mwa huduma yake kama Petro. Akachukuliana na wabaya (wayahudi) hao hao aliwahukumu hawataingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya sheria.
Oct 17, 20255 min read


KANISA LA MUNGU/KRISTO KATIKA NYAKATI SABA.
Hivyo makanisa saba ni nyakati saba za kanisa la Kristo, yaani kanisa moja linapita katika majira saba ya kutakaswa kwake. Kila wakati kanisa linapopokea ufunuo wa Mungu na kutoka hatua moja kwenda nyingine, linapotoka linaacha dhehebu ambalo halikuamini ufunuo wa Mungu uliokuja kuwatakasa ili kwenda hatua inayofuata.
Oct 17, 20254 min read


KANISA LA MUNGU/KRISTO NI LIPI?
Hivi ndivyo kanisa linageuka kuwa dhehebu, likiisha kukataa kupokea ufunuo wa Mungu, linabaki kama dongo la fedha (fedha pamoja na udongo wake). Yeremia alihubiri kanisa lile wakubali kusafishwa, waondoe uchafu wao, nao wakakataa wakijiona wanalo neno la Mungu. Lakini walikuwa kama dongo la fedha wala si fedha yenyewe, naam hawakuwa katika matumizi yoyote maana fedha isiposafishwa haina matumizi.
Oct 16, 20256 min read


KURUDI KWA YESU KRISTO MARA YA PILI NI PIGO LIFURIKALO
Kurudi kwa Kristo ni kitendawili kigumu, hasa katika nyakati hizi. Kulingana na ufunuo wa damu na nyama unaoongoza kanisa la wakristo,...
Sep 12, 20256 min read


KUPATWA KWA MWEZI HUMAANISHA NINI KATIKA ROHO?
Jana tarehe 7 ya mwezi huu wa 9, 2025 limeonekana tukio la nadra sana kutokea, mwezi ulikuwa kama damu. Tukio hili huitwa kupatwa kwa...
Sep 8, 20253 min read


UFUNUO NA INJILI YA NYOKA.
Shalom, Karibu katika Neno la Mungu, Bwana na akujalie kula chakula kigumu, kwa kuwa nimeshuhudiwa hakika ya kuwa mngali watoto wadogo...
Aug 22, 20257 min read


TUNDA GANI ADAMU NA HAWA WALIKULA?
Tunda hili lilikuwa chanzo cha mauti kwa mwanadamu, Baba yetu Adamu na mama yetu Hawa walikula tunda hili wakaleta mauti duniani. Lakini tunda hili lipo hata sasa na kanisa na watu wote jamii wangali wakilila.
Shalom, Karibu tena katika Neno la Mungu. Na moja kwa moja tutazame habari hii katika kitabu cha Mwanzo 2:16-17
Aug 18, 20254 min read


KALAMU YA UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA BIBLIA KUWA UONGO
Shalom, Karibu katika Neno la Mungu, na moja kwa moja tusome maandiko katika Yeremia 8 8 Mwasemaje, Sisi tuna akili, na torati ya Bwana...
Aug 9, 20253 min read


UFUNUO WA DAMU NA NYAMA NA UFUNUO WA MUNGU
Shalom, Karibu katika Neno la Mungu, hekima ya Mungu ikupayo uzima. Kanisa au dini yoyote na hata katika Elimu ya ulimwengu huu...
Aug 6, 20254 min read


HATA SASA MNGALI MKIHITAJI MAZIWA
12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu.
13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga.
14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.
Aug 1, 20254 min read
bottom of page